Monday, January 6, 2014

MAELFU WAMZIKA DR.MGIMWA.

Naibu  spika  Job Ndungai  akiweka  mchanga  katika kaburi ya  Dr Mgimwa
Mjane  wa Dr Mgimwa akiaga  mwili  huo kabla ya mazishi kijiji   cha Magunga  Iringa  leo 
Mwili  wa Dr Mgimwa ukishushwa kaburini  leo 
Wabunge  Deo  Sanga  wa jimbo la Njombe Kaskazin  kushoto na Deo Filikunjombe wa Ludewa  
rais  Kikwete na mkewe  wakiweka  shada la maua 
MAELFU   ya  wakazi  wa mkoa  wa Iringa na  baadhi  ya  viongozi  wa  vyama  vya  siasa na  Serikali  wakiongozwa na  Rais Dr  Jakaya  Kikwete  wameshiriki  katika mazishi ya  aliyekuwa  mbunge wa   jimbo la Kalenga na  waziri wa fedha  Dr  Wiliam Mgimwa.

Huku   waziri  mkuu Mizengo  pinda katika  salam  zake za serikali akielezea  jinsi ambavyo  Taifa  lilivyopata  pigo kubwa  kufuatia  kifo  cha Dr Mgimwa kutokana na mchango  wake  katika baraza la mawaziri.

Katika  mazishi  hayo   yaliyofanyika  leo kijiji  kwake Magunga  jimbo la Kalenga   wananchi   mbali  mbali   walionyesha  kujipanga  barabarani  kutoka Manispaa ya  Iringa  hadi  kijijini kwake  huku  wakiupungia mkono msafara  wa    rais Kikwete na baadhi yao  wakilazimika  kutumia  usafiri wa baiskeli na pikipiki  kwenda katika mazishi  hayo.

Akitoa   shukrani za  familia kwa niaba ya  familia  mtoto wa marehemu Dr Mgimwa Godfrey  Mgimwa  aliishukuru   serikali kwa  jinsi ambavyo ilivyohangaika  kumuuguza baba  yake  na  kutoa wosia  mzito wa marehemu  Dr Mgimwa ambao  alimtaka kuufikisha kwa Rais  Kikwete..

Alisema  katika  uhai  wake kabla  ya kifo  chake  ikiwa ni siku tano kabla  Dr  Mgimwa alimwita na  kumtaka  kufikisha  shukrani zake kwa Rais  Kikwete kwa  kumtembelea mara mbili Hospital  alipokuwa amelazwa  pamoja na  spika wa bunge Anne makinda .

Pia  alisema  kuwa alieleza dhamira  yake ya  kuwatumikia  wana Kalenga na  kusema  zawadi kubwa ni msaada wa bati  zaidi ya  2000 kwa wananchi hao  ili kuendeleza ujenzi wa shule na  vituo  vya afya  jimboni.

"Baba  kabla ya  kufa  aliniachia  wosia  huo juu ya wana Kalenga kwa kuwashukuru kwa  ushirikiano  wao na  kutoa  bati ila alipenda  kuona  Kalenga  inakuwa na maendeleo zaidi"

Kwa  upande  wake  waziri Mkuu Pinda  alisema  kuwa  serikali imepata pigo kubwa  juu ya kifo hicho na kuwa  bado serikali  itaendelea  kuwa karibu na familia ya Dr Mgimwa  na pale  penye tatizo  isisite  kuwasiliana .

Hata  hivyo  Rais  Kikwete  hakupata  kuzungumza  chochote  katika msiba  huo  zaidi ya  kuweka mchanga na shada la maua pamoja na kuwapa mkono  ndugu wa Dr Mgimwa .


Spika  wa bunge Anne Makinda  alisema kuwa  bunge  limempoteza kiongozi na mbunge aliyependa kutumia  nafasi yake kwa ajili ya Taifa  na kuwa kamwe mchango  wake  hawataacha kuukumbuka.
CUF HAIHUSIKI NA NJAMA ZOZOTE DHIDI YA CHADEMA KWENYE SAKATA LA ZZK;


Wadau, waandishi wengi wa habari wananipigia nithibitishe ikiwa CUF iliandaa makundi ya wanachama wakamshabikie ZZK mahakamani leo hii. Taarifa ya namna hii pia imeenea mitandaoni.

Pia viongozi kadhaa wa CHADEMA wamenipigia kunijulisha kuwa Intelijensia yao imegundua kuwa vijana wa CUF wamepenyezwa na kwamba wamevushwa T-SHIRT za M4C na mapanga.

Napenda kuwajulisha wadau wote kuwa CUF haijapanga wala kutuma makundi ya vijana kwenda kumshabikia ZZK. Ikiwa pana wanachama wa CUF wameonekana mahakamani itakuwa wamekwenda kwa Utashi na Matakwa yao.

Sisi chama Taifa hatujawahi kukutana, kupanga wala kutuma vijana wa CUF wakasimamie upande wowote katika mgogoro huu. Wakati wa fukuto la HAMAD RASHID na CUF watu wengi tu raia walifika mahakamani, sie hatukuwa kuhoji na kutafuta vyama vyao, tuliamini ni watanzania tu.

Ni ushauri wangu kuwa, panapokuwa na kesi inayovuta hisia za watu haitajalisha watu hao wanatoka makundi gani, mwenye kutaka kwenda atakwenda tu.

Ni vigumu kwa chama chetu kukataza wanachama wake wasihudhurie kesi ya Babu Seya, ya Sheikh Ponda, ya Zitto Kabwe, ya Samaki wa magufuli n.k., Unapokuwa na chama chenye mamia elfu ya wafuasi si rahisi kujua mfuasi yupi yuko wapi kwa wakati gani anafanya nini na ametumwa na nani.

Lakini kwa ajili ya kujenga mshikamano wa vyama vyetu, tunachunguza taarifa hizo ili kubaini kama ni kweli palikuwa na wanachama wetu mahakamani na tukiwabaini tutawahoji na kujua nani aliyewatuma na tutaona hatua za kuchukua.

Ikumbukwe kuwa mwenyekiti wa chama chetu taifa Prof. Lipumba wakati akisoma maazimio ya kikao Cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa mwezi Desemba mwaka jana alieleza kuwa Baraza Kuu la CUF linawaomba CHADEMA wamalize mgogoro wao haraka ili tuwekeze nguvu za upinzani katika kuunganisha umma kutafuta katiba ya watanzania katika bunge la katiba, Msimamo wa CUF ni kutokuwa na upande katika mgogoro huu.


Tunatoa wito kwa viongozi wa CHADEMA kutoa taarifa kwa vyombo vya ulinzi na usalama iwapo wataona au kuhisi kuna mwananchi au mfuasi wa chama chetu amejiingiza katika mgogoro wao na kwamba amehatarisha amani ili sheria ichukue mkondo wake.

CUF itaendelea kuiheshimu CHADEMA kama taasisi inayojitegemea. Hatukuwahi kuingilia, kushabikia wala kupinga masuala na maamuzi ya ndani ya CHADEMA, tukiona pana jambo linatugusa mara zote huwa tunatoa ushauri wetu tu na sio kuingilia masuala ya ndani ya vyama vingine.

________________________________
Julius Mtatiro,
National Deputy Secretary General,
The Civic United Front(CUF),
Tanzania Mainland,
P.O Box 10979,
Dar Es Salaam.
Phone; +255717536759,



                       RADIO ICE FM 99.3MHz PROFILE

Radio ICE FM is wholly owned by indigenous Tanzanians and transmits its programmes from Mjimwema in Njombe District where is primarily founded. The company “Ice Intertainment and Promotion Co.Ltd” was incorporated in 3rd March 2012 with registration number 86136. Registration of this Radio station is in line with the national policies and laws that made room liberalization of media and publicity industry from early 1992.
Since its lawfully authorized inception to broadcast to date, Radio ICE FM has consistently broadcast programmes to the targeted audience within the specified frequencies or boundaries in Kiswahili. Radio ICE FM is a 24 hours broadcasting services.
Radio ICE FM is licensed by Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) as commercial service broadcaster with a mandate to provide service from base station in Makambako. The coverage of Radio ICE FM is spreading, in the former media undeserved areas of Makambako, Njombe,Makete, Mafinga, rural Iringa,Kilolo District,Wanging’ombe district, Chimala(Mbeya),Mbalali (Mbeya), ,. The coverage spreads to the parts of , Ulanga District(Morogoro), Mpwapwa (Dodoma), and Manyoni (Singida) within six regions and powered by 1 kW transmitters in Mama Clementina Hill – Makambako. It is of interest to note that in the area of Mchuchuma and Liganga, mining sites with prospects of massive industrial activities in the nearest future. Our equipment out-perform other broadcasters in similar category reaching ten (10) districts spanning six regions of Njombe,Iringa, Mbeya ,Dodoma,Singida and Morogoro.
From the above facts, it is undoubtedly clear that Radio ICE FM is one of few radio stations with the real touch of the community and broadcasting from Small Township to bigger townships and localities which makes it unique in its class.
Radio ICE FM technical secretariat derives its visions and guidance from the Board of Directors which is currently led by the Board Chairperson. The secretariat is led by the Manager who is supported by key technical personnel of presenters, DJs, producers, editors, programmer and others. Management has the responsibility of complying with the rules and regulations as provided by TCRA.


FORMAT AND BROADCASTING
Radio ICE FM broadcasts in Kiswahili, 24 hours a day. It has a range of routine programs comprising of music coupled with extensive news and features coverage.



Radio ICE FM, P. O. Box 188, Iringa. e-mail: icemedia8@gmail.com  mob. +255 753 808722
National news  is 21.00 pm daily. Radio ICE FM news team compiles local news from Southern Highland zone and other region.The station has a dedicated team of news reporters equipped to obtain some live local events outside the station. Features content focusing community development and empowerment of women and other periphery groups like children and disabled, environmental issues etc. Programmes on HIV/AIDS education are given greater emphasis. Peak audience periods are between 6am – 9am and 18pm – 21pm. News and sports content is sourced from a range of domestic and international sources including Voice of America who are our partner broadcaster.

TECHNICAL CAPACITY
ICE FM has the capacity to produce Radio programs both in the field and post production suites at Mjimwema studios. This is made possible by deployment to the field of very portable audio recording equipment. This  equipment is easy to operate leaving the presenter or resource person to concentrate on the contents of the recording. The recorded material is then brought back to the studios for post-production where it is edited to remove unsuitable material and condensed to fit the program duration. Sound effects and signature tunes are also added and the whole program packaged using digital technology. The digital technology consists of non-linear editing equipment using the best audio editing software. The broadcast studies are integrated and equipped with computerized music and format control systems. In addition, we have integrated production facilities capable of content storage and retrieval. The production team produces all program imaging in house as well as offering advertisers production facilities.
Radio ICE FM, P. O. Box 188, Iringa. e-mail: icemedia8@gmail.com  mob. +255 754605723